Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amemtangaza Khalifa Suleiman Khalifa kuwa katibu mkuu wa chama hicho akichukua nafasi ya Maalim Seif Sharrif Hamad.
SIKU moja baada ya mahakama kuu ya Tanzania, kutoa hukumu ya kuusafisha uenyekiti wa Prof. Ibrahim Lipumba katika chama cha CUF, mwenyekiti huyo amewataka wanachama wa chama hicho hasa Zanzibar kuacha jazba.
Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi CUF, Prof Ibrahim Lipumba amewaomba wanachama wa chake upande wa Zanzibar kuendelea kusalia kwenye chama hicho licha ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Sharif kutangaza kuhamia ACT - Wazalendo.